Matthew 24:29-35

Kuja Kwa Mwana Wa Adamu

(Marko 13:24-31; Luka 21:25-33)

29 a “Mara baada ya dhiki ya siku zile,

“ ‘jua litatiwa giza,
nao mwezi hautatoa nuru yake;
nazo nyota zitaanguka kutoka angani,
na nguvu za anga zitatikisika.’
30 b “Ndipo itakapotokea ishara ya Mwana wa Adamu angani, na makabila yote ya dunia yataomboleza. Nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya angani, katika uwezo na utukufu mkuu. 31 cNaye atawatuma malaika zake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwisho mwingine.

32 d “Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 33 eVivyo hivyo, myaonapo mambo haya yote, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni. 34 fAmin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia. 35 gMbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Copyright information for SwhNEN